
Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Kisii (KTRH) ambako waandamanaji waliopigwa mshale walikimbizwa kwa matibabu. Picha|Wycliffe Nyaberi[/caption] "Baadhi ya wanasiasa walikodi wahuni na kuwaweka katika maeneo mbali mbali ili kutufuata. Wahuni hao walikimbia kujificha katika majengo yanayositiri afisi za mwanasiasa mmoja kutoka eneo hili. Waandamanaji walipokuwa wakipita karibu na afisi hizo, waliwafyatulia mishale. "Hata hivyo, hilo halitazuia harakati zetu za kupigania utawala bora wa nchi hii," alisema Bw Sammy Nyakundi, mkazi wa Kisii. Vijana walianza kumiminika katika mitaa ya mji wa Kisii mapema kuanzia saa mbili asubuhi. Walianza kwa kuyageuza makutano ya Capital mjini Kisii uwanja wa kuruka kamba, kucheza kandanda na michezo mingine ya kukimbizana. Baadaye, waliwasha moto na kuziba barabara kuu zinazoingia na kutoka Kisii. Polisi walipoona wanaziba barabara hizo, walianza kuwatawanya kwa kuwarushia vitoa machozi. Biashara nyingi zilisalia kufungwa kutwa nzima katika mji huo.from Taifa Leo https://ift.tt/PGTDKSN
via IFTTT
Tags
TRENDING NEWS